Mafunzo na Mafunzo mapya

Mafunzo, Mfanyakazi, Ustadi, Ujuzi, Kazi, Maarifa, Mawakala, Mashirika, Wafanyakazi, Masomo, Elimu, Taasisi, Shirika, Waajiri, Tanzania, Chama, Mishahara, Cheo, Mpya, Ratiba.

Je, kwa nini nipate mafunzo au mafunzo mapya?

Kuna sababu kadhaa ambazo zinaweza kumfanya mfanyakazi kupata mafunzo au mafunzo mapya. Baadhi ya hizi ni pamoja na: shinikizo la kupigwa kalamu, hitaji la kuboresha ustadi ili kulingana na mahitaji ya kikazi, tamaa ya kubadilisha kazi, matarajio ya kutafuta nafasi mpya; na pengine kupata cheo. Mfanyakazi anapaswa kuzingatia mafunzo wakati wowote anapokabiliana na moja kati ya hali zilizo hapa kuu.

Je, mafunzo au mafunzo mapya ni nini?

Mafunzo au mafunzo mapya katika hali hii hurejelea kuboresha ustadi wa mtu ikilinganishwa na mahitaji ya kikazi au tamaa ya kutafuta kazi mpya. Kwa hivyo ni kitendo cha kuongeza maarifa katika ufahamu na ustadi wa mtu.

Je, inafaa kuwekeza katika mafunzo yangu mwenyewe au ninapaswa kumtegemea mwajiri wangu?

Mafunzo yako ni kama uwekezaji – utapata faida ya uwekezaji kama huo. Licha ya hiyo, unashauriwa kuwekeza katika mafunzo na mafunzo yako mapya mara nyingi kama uwezavyo.

Je, mwajiri anaweza kulipia mafunzo yangu?

Ndiyo. Waajiri wengi hupanga na kulipia mipango ya mafunzo mapya ambayo yanafanywa na mawakala/mashirika mengi kwa wafanyakazi wao. Ikiwa una meneja wa mafunzo au afisa anayewajibika kwa wafanyakazi katika mahali pako pa kazi, mweleze mahitaji yako ya mafunzo. Jaribu kulinganisha mahitaji yako ya mafunzo na mahitaji yako ya kazi ili yawe yanaongeza thamani kila wakati kwa kile unachokifanya.

Je, ni kwa nini nipate mafunzo au mafunzo mapya?

Huenda ukataka kupata mafunzo/kufunzwa upya ili uboreshe ustadi wako wa mahitaji yako ya kazi, au pengine kujiandaa mwenyewe kwa kazi mpya. Ikiwa unahisi kwamba una upungufu wa ustadi fulani ambao unahitajika katika kazi yako, basi nenda upate mafunzo ya ustadi huo. Ikiwa unataka kubadilisha kazi lakini unakosa ustadi unaohitajika, fanya hivyo pia.

Je, ni wakati upi unaofaa kwa mafunzo?

Hakuna kipindi maalum kinachofaa cha mafunzo kama hayo. Inategemea kwa sana upatikanaji wako, rasilimali na upatikanaji wa mpango unaohitajika wa mafunzo kutoka kwa mtoa huduma anayependelewa wa mafunzo. Kwa hivyo mtu hafungwi na muda – haya sio mafunzo rasmi ambapo mtu ana ratiba kama vile vyuo vya elimu au vyuo vikuu.

Je, kuna taasisi au mashirika gani ya mafunzo yanayohusiana na kazi nchini Tanzania?

Nchini Tanzania kuna taasisi au watoa huduma kadhaa wa mafunzo ya muda mfupi au muda mrefu wanaolenga wafanyakazi na hata ngazi za usimamizi.  Shirika la Waajiri wa Tanzania (ATE) Na Chama cha Wafanyakazi wa Tanzania (TUCTA) ndizo taasisi kubwa kabisa zinazotoa mafunzo kama hayo.

Soma zaidi

Fanya Uchunguzi wetu wa Mishahara na uchangie uwazi wa mishahara nchini Tanzania.

Loading...