Majukumu ya kifamilia

This page was last updated on: 2023-05-21

Likizo ya uzazi kwa Mwanaume/ baba

Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini 2004 inatoa likizo ya malipo ya uzazi kwa baba kwa angalau siku 3 (katika kipindi cha likizo cha miezi 12) kwa baba mgebi ikiwa likizi hii itachukuliwa katika siku 7 za kuzaliwa kwa mtoto.

Mwajiri anaweza kuhitaji uthibitishaji usio na shaka wa kuzaliwa kwa mtoto kabla ya kulipia likizo ya uzazi kwa baba. Mfanyakazi lazima awe ameajiriwa na mwajiri husika kwa kipindi kisicho pungua miezi sita katika miezi 12 kabla ya kuzaliwa mtoto au awe ameajiriwa kwa mkataba wa kazi maalumu na mwajiri husika.

Chanzo: § ya 34 ya Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya 2004; ISSA Nchi ya Tanzania, 2017

Likizo ya malezi ya mtoto

Sheria haina kifungu kinacho elezea kwamba baba apewe likizo ya uzazi yenye malipo au isiyo na malipo.

Kazi mbadala zinazoruhusu kukidhi majukumu ya kifamilia kwa mfanyakazi mwenye mtoto mchanga

Hakuna kifungu cha sheria kinacho ruhusu mfanya kazi kukidhi mahitaji ya kazi na familia hususani anapokuwa na mtoto mchanga.

Taratibu juu ya mfanyakazi na majukumu ya kifamilia

  • Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Sehemu ya 6 ya 2004 / Employment and Labour Relations Act, No. 6 of 2004
Loading...