Utumikishaji wa Watoto

This page was last updated on: 2023-05-18

Watoto chini ya miaka 15

Umri wa chini wa ajira ni miaka 15 na juu. Mtoto wa miaka 15 na juu anaweza kufanya kazi ambayo ni rahisi ambayo haidhuru afya au kukua kwa mtoto, hakuzuii au kuathiri mtoto kwenda shule, kuhusika katika mafunzo ya utaalamu au mpango wa mafunzo au uwezo wa mtoto kufaidika na kazi ya shule. Mtoto (chini ya umri wa miaka 15) huenda asiajiriwe katika aina yoyote ya kazi isipokuwa kazi ya nyumbani (kazi katika nyumba ya familia).

Mtu anayemwajiri mtoto kwa kukiuka toleo hili ana hatia ya kosa na anawajibika, baada ya kushtakiwa, kulipa faini ya shilingi milioni 0.5 hadi 02 au kifungo cha kipindi cha miezi 12 hadi miaka 02 au zote pamoja na kifungo.

chanzo: §97, 98 na 106 ya Sheria ya Watoto 2011; §06-08 ya Sheria ya Ajira Nambari 11 ya 2005  

Umri wa chini kwa kazi hatarishi

Umri wa Chini wa Kazi Hatari umewekwa kama miaka 18 na hakuna yeyote anaweza kuwaajiri watoto chini ya umri wa miaka 28 kwa kazi hatari au ya aina yoyote inayohatarisha watoto (utumwa, ufungwa, kuwatumia watoto kwa ukahaba na malengo ya ponografia, kuwatumia watoto kwa uzalishaji na ulaguzi wa dawa za kulevya, na kazi ambayo inaweza kudhuru afya, usalama na maadili ya watoto.

Sheria ya Watoto imepiga marufuku kuwahusisha watoto katika shughuli za kuwatumia vibaya. Shughuli ya kikazi huwa kazi ya kuwatumia vibaya ikiwa inamnyima mtoto afya au kukua kwake, inazidisha saa sita kwa siku, haifai umri wa mtoto au ukuzaji au uhitaji mtoto kufanya kazi usiku (kuanzia saa 20:00 hadi 06:00 asubuhi).

Sheria ya Watoto imepiga pia marufuku kuwaajiri watoto katika kazi hatari (kazi ambayo ina hatari kwa afya, usalama na maadili ya mtu). Kazi hatari hujumuisha uchimbaji na upasuaji mawe, kubeba mizigo mizito, kufanya kazi katika viwanda vya utengenezaji ambapo kemikali huzalishwa na kazi yoyote hatari kama ilivyotangazwa na serikali.

 Mtu anayemwajiri mtoto kwa kukiuka toleo hili ana hatia ya kosa na anawajibika, baada ya kushtakiwa, kulipa faini ya shilingi milioni 0.5 hadi 02 au kifungo cha kipindi cha miezi 12 hadi miaka 02 au zote pamoja na kifungo.

chanzo: §99, 100 na 106 ya Sheria ya Watoto 2011; §06-08 ya Sheria ya Ajira Nambari 11 ya 2005 

Loading...