MKATABA WA HALI BORA WA KAZI BAINA YA CHAMA CHAWAFANYAKAZI WA VIWANDA, BIASHARA, TAASISI ZA FEDHA, HUDUMA NA USHAURI (TUICO) NA SAID SALIM BAKHRESA & CO. LTD (MZIZIMA)

New1

1. UTANGULIZI

Mkataba huu unajulikana kama Mkataba wa Hali Bora unaohusisha masuala ya ajira na mahusiano kazini kati ya mwajiri yaani Said Salim Bakhresa & Co Ltd (SSB & CO. LTD) na tawi la chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) yaani wawakilishi wa wafanyakazi.

Kwamba sisi SSB &Co Ltd tujulikanao kama mwajiri kwa upande mmoja na Tawi la chama cha wafanyakazi wa viwanda, biashara, taasisi za fedha, huduma na ushauri ( TUICO) Tawi la chama cha wafanyakazi kwa upande mwingine tunakubaliana mambo yafuatayo:

- Kwamba kwa hiyari yetu wenyewe tumekubaliana mambo yafuatayo;-

- Kwamba mwajiri anatambua kuwa TUICO ndicho chombo ambacho kinawakilisha wafanyakazi katika masuala ya utetezi na maslahi ya wafanyakazi kwenye Kampuni yake.

- Kwamba TUICO inatambua kuwa SSB & Co Ltd (Mzizima) ndiye mwajiri aliyewaajiri wafanyakazi wanachama wa TUICO na ana mamlaka kuhusu ajira na maslahi ya wafanyakazi.

2. KIMA CHA CHINI CHA MSHAHARA

Pande zote mbili zimekubaliana kwamba kima cha chini cha mshahara ni Tsh 150,000/=(Laki moja na elfu hamsini tu) kuanzia tarehe 01. 03. 2012.

3. LIKIZO

Pande zote mbili tumekubaliana kuwa

Kila mwaka mfanyakazi atakuwa na haki ya kwenda likizo na atakuwa na haki ya kupata Tsh 120, 000/=(Laki moja na ishirini) wakati atakapo kuwa anakwenda likizo yake ya mwaka (Annual leave), malipo ambayo yatajulikana kama posho ya likizo (leave allowance). Utaratibu huu pia utaanza kutumika 01. 03. 2012.

4. KIFO

Pande zote mbili tumekubaliana kwamba:

i. Endapo mfanyakazi atafariki mwajiri atatoa Tsh 500, 000/- ambazo ubani na gharama za mazishi.

ii. Endapo mfanyakazi atafiwa na mke, mume, mtoto wa kumzaa mwenyewe, baba mzazi, au mama mzazi,

mfanyakazi huyo atapewa rambirambi ya Tsh 200, 000/=(Laki mbili tu)

5. MFANYAKAZI HODARI

Pande zote mbili tumekubaliana kwamba:-

i. Inapofika wakati wa sherehe ya sikuu ya Mei Mosi kila mwaka mwajiri atakuwa na haki ya kutoa mfanyakazi hodari ambaye atakuwa anachaguiiwa kwa kushirikiana na Tuico na Mwajiri.

ii. Mfanyakazi bora wa kampuni atazawadiwa na mwajiri Tsh 500, 000/=(Laki tano)

iii. Mfanyakazi bora wa idara atazawadiwa na mwajiri Tsh 200, 000/=(Laki mbili)

6. MUDA WA MKATABA

Pande zote mbili tumekubaliana kuwa muda wa mkataba ni miaka miwili (2) kuanzia tarehe 1/3/2012 mpaka tarehe 1/3/2014

7. MASURUFU (ALLOWANCES)

i. Kodi ya nyumba Tsh 40, 000/= kila mwezi

ii. Nauli Tsh 30, 000/= kila mwezi

8. MENGINEYO

Pande zote mbili tumekubaliana kwamba:-

i. TUICO watazingatia kanuni na sheria zote za kazi za hapa nchini.

ii. Wafanyakazi watazingatia kuwa lazima wafikie lengo la ubora wa bidhaa na kuzalisha kwa kiwango cha juu cha mashine (Quality products and full capacity of machine)

9. HITIMISHO

Mkataba huu umethibitishwa na kusainiwa leo tarehe .../.../ 2012

Kwa upande wa TUICO:

Kwa upande wa Mwajiri:

Umesainiwa kwa niaba ya SAID SALIM BAKHRESA & CO. LTD:

Jina

Jina…………………………………………………..

Sahihi

Cheo

TZA Said Salim Bakhresa and Co. Ltd (MZIZIMA) - 2012

Start date: → 2012-03-01
End date: → 2014-03-01
Ratified by: → Ministry
Ratified on: → Not yet ratified
Name industry: → Manufacturing
Name industry: → Manufacture of beverages
Public/private sector: → In the private sector
Concluded by:
Name company: →  Said Salim Bakhresa and Co. Ltd (MZIZIMA)
Names trade unions: →  Chama Chawafanyakazi Wa Viwanda, Biashara, Taasisi Za Fedha, Huduma Na Ushauri (TUICO)

WORKING HOURS, SCHEDULES AND HOLIDAYS

Paid annual leave: → Not specified days
Paid annual leave: → Not specified weeks
Provisions on flexible work arrangements: → 

WAGES

Wages determined by means of pay scales: → No
Provision that minimum wages set by the government have to be respected: → 
Adjustment for rising costs of living: → 0

Extra payment for annual leave

Extra payment for annual leave: → TZS 120000.0

Allowance for commuting work

Allowance for commuting work: → TZS 30000.0 per month

Meal vouchers

Meal allowances provided: → No
Free legal assistance: → 
Loading...