Afya na Usalama Mahali pa Kazi

This page was last updated on: 2023-05-21

Wajibu wa mwajiri

Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa kazi, 2003 inamtaka mwajiri kutoa mazingira yenye afya, usalama na ustawi kwa wafanyakazi wake wote na kuhakikisha kurudi kwa maisha ya kawaida kwa wafanyakazi walioathiriwa. Ni lazima mmiliki kutoa na kuendeleza kifaa na mifumo na utaratibu wa kazi ambao ni salama na bila hatari kwa afya ya wafanyakazi. Mwajiri lazima ahakikishe usalama na kutokuwepo na hatari ya kiafya katika utumizi, shughuli, uwekaji na usafirishaji wa kikorokoro na mali. Utoaji wa maelezo, agizo, mafunzo na usimamizi kama huu kwa wafanyakazi ni muhimu sana ili kudumisha usalama na afya katika mahala pa kazi. Njia ya kufikia na kutoka mahala pa kazi panafaa kuwa salama na bila hatari. Hatua za hadhari zinafaa kuchukuliwa ili kuondoa au kupunguza hatari zozote au hatari inayowezekana kwa usalama na afya ya wafanyakazi.

Lazima vifaa vya usalama kutolewa na kudumishwa katika kila eneo la kazi. Kamwe wafanyakazi wasihatarishwe kwa mnururisho; vitu vinavyowasha; mashine na vifaa hatari; au wanyama na wadudu na hatari; au ajenti zinazo ambukiza au mizio; au kemikali hatari; au mazingira hatari wakati wa kufanya kazi kama mafanyakazi wa kilimo.

Mahali pa kazi na mazingira ya kazi ambayo ni salama, bila hatari ya afya na vifaa vinayotosha na mipango ya ustawi wa wafanyakazi kazini unafaa kudumishwa. Wafanyakazi wanafaa kujulishwa vyema kuhusu hatari yoyote ambayo inaweza kutokea na wanastahili kushiriki katika utendaji na ukaguzi wa hatua za usalama na afya.

Lazima mwajiri pia ahakikishe usafi unaostahili; utoaji wa maji safi ya kukunywa; vyoo vya umma vya kutosha na vinavyostahili; vifaa vya kutosha vya kuoshea; mahala pa mavazi; vifaa vya huduma ya kwanza; na mahali panapofaa pa kuketi wakati wa mapumziko.

Hatua za kuzuia na kulinda zinafaa kuchukuliwa baada ya ukadiriaji unaofaa wa hatari (angalau mara moja kwa mwaka) ili kuhakikisha ya kwamba kemikali, mashine, zana na njia zote ni salama na bila hatari kwa afya na zinafuata mahitaji ya sehemu ya usalama na afya katika sheria hii.

Lazima wafanyakazi watumie vifaa vya usalama kwa uangalifu na kufuata maagizo yaliyoamuriwa ili kudumisha afya yake na kumlinda dhidi ya kuumia. Kamwe mfanyakazi asihusike katika kitendo chochote ambacho kinazuia utekelezaji wa maagizo au matumizi mabaya au kusababisha uharibu au kupotea kwa njia zilizotolewa za ulindaji, usalama na afya ya wafanyakazi wengine. Lazima aripoti kwa mwajiri au msimamizi wa afya na usalama ikiwa hali dhaifu au isiyo salama itatokea.

Chanzo: §54-61, 65-76, 95 & 99 Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa kazi 2003

Kukingwa Bure

Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa kazi 2003 inahitaji waajiri kutoa kifaa cha kulinda (PPE) kwa wafanyakazi wanaohusika katika kazi hatari.

Ni lazima mwajiri atoe kifaa cha kinachofaa cha kulinda ikiwa wafanyakazi wanaachwa wazi kwa mazingira ya kuumiza au kifaa cha kudhuru. Aina ya PPE inayohitajika inatofautiana kulingana na kazi inayotekelezwa.

Sehemu ambayo vitu vyenye sumu vinazalishwa, kutunzwa au kuhifadhiwa, Mkaguzi Mkuu anaweza kumtaka mwajiri kutoa huduma za ziada kama mahali ya kuogea, kuandaa uchunguzi wa mara kwa mara wa afya toka kwa taasisi inayokubalika ikiwa ni pamoja na kutoa mavazi ya kujikinga.

Waajiri hawaruhusiwi kupunguza kiwango chochote kutoka kwa mishahara ya wafanyakazi ili kumpa chochote katika kufuata Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa kazi.

Chanzo: §62, 63, 67(6) & 94 Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa kazi 2003

Mafunzo

Kwa mujibu wa Sheria ya Afya na Usalama sehemu ya Kazi 2003, ni wajibu wa mwajiri kutoa maelezo, mafunzo na usimamizi kadri inavyohitajika ili kuhakikisha afya na usalama kazini kwa wafanyakazi wake. Kila mfanyakazi aeliemishwe (juu ya) kazi anayofaa kutekeleza, nyenzo au kifaa atakachotoa, kuzalisha, au kusafirisha au mashine yoyote anafaa kuendesha. Lazima mafunzo yatolewe mara moja ndani ya miaka miwili. 

Chanzo: § 34 & 95 ya Sheria ya Usalama na Afya Kazini, 2003

Mfumo wa Kukaguliwa na Mkaguzi wa Ajira

Sheria ya Usalama na Afya Kazini, 2003 inatoa mfumo wa kusisimua wa ukaguzi wa ajira. Tanzania Bara na Zanzibar kuna mfumo unaojitegemea wa ukaguzi wa ajira. Hata hivyo, mfumo wa ukaguzi ni wa wilaya na hakuna mamlaka ya kati ya ukaguzi.

Wizara ya Ustawishaji Ajira, Vijana na Ajira (MoLEYD) inawajibu wa ukaguzi wa ajira. Ukaguzi umegawanywa kati ya maafisa wa ajira wanaofanya kazi MoLEYD (hiyo ni, kuangalia mikataba ya ajira, mishahara, masaa ya kufanya kazi nk.) na wakaguzi wa usalama na afya kazini ambao ni sehemu ya Weledi ulio huru wa Usalama na Afya Kazini (OSHA). Taasisi zingine za serikali kama vile Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii pia hufanya ukaguzi huru lakini na uratibu wa chini na MoLEYD au OSHA.

Wakaguzi wa ajira wameidhinishwa kutekeleza sheria ya ajira, kutoa maelezo na ushauri kwa waajiri na wafanyakazi kuhusu jinsi ya kutii sehemu za sheria ya ajira pia kujulisha mamlaka halali kuhusu mwenendo wowote mbaya au unyanyasaji ambao hushughulikiwi na sehemu zilizopo. Pia wakaguzi wa ajira pia huchukua wajibu mwingine ikiwa ni pamoja na kutatua mzozo.

Utungaji sheria wa kitaifa huwapa wakaguzi uwezo wa kuingia, kukagua na kuchunguza mahali pa kazi wakati wowote usiku au mchana na au bila notisi ya kabla; kuchukua hatua, picha, hati, vyeti na notisi za kukagua, kuchunguza na kuzinakili; kuhoji yeyote; ikiwa mkaguzi ni daktari anaweza kufanya uchunguzi wa tiba; na anaweza kwenda na afisa wa polisi ikihitajika.

Ikiwa mmiliki au wawakilishi wake hawatamsaidia mkaguzi na kuzuia utendaji wa wajibu wake, anafanya makosa na anawajibika kisheria kwa faini ya hadi shilingi milioni 2 au kifungo gerezani cha hadi miezi mitatu au zote.

Chanzo: § 6-10 Sheria ya Usalama na Afya Kazini, 2003

Taratibu juu ya Afya na Kazi

  • Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa kazi mwaka 2003 / Occupational Health and Safety Act, 2003
Loading...